Madhambi yanamfanyia mambo kuwa mazito yule mtenda dhambi. Hakuna jambo analotaka kulifanya, isipokuwa ataona milango yake imefungwa au gumu kuliendea. Hili ni kama vile ambavyo yule ambaye anamcha Allaah atayaona mambo yake kuwa mepesi. Yule mwenye kuacha taqwa basi atayaona mambo yake kuwa magumu. Ee Allaah! Ni ajabu iliyoje pindi mtu anapoona milango ya kheri na ya manufaa imefungwa na milango ya kuiendea ni migumu pasi na kujua yote hayo yamesababishwa na nini!

  • Mhusika: Imaam Ibn Qayyim-il-Jawziyyah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Daa’ wad-Dawaa’, uk. 66
  • Imechapishwa: 30/12/2017