05. Dalili juu ya mguu wa Allaah 5

5- Abu ´Abdillaah al-Mu´addil Ahmad bin ´Umar bin ´Uthmaan ametuhadithia tulipokuwa Waasitw: ´Iysaa bin Abiy Harb ametuhadithia: Yahyaa bin Abiy Bukayr ametuhadithia: ´Abdul-Ghaffaar bin al-Qaasim ametuhadithia: ´Adiyy bin Thaabit amenihadithia: Zirr bin Hubaysh amenihadithia, kutoka kwa Ubayy bin Ka´b aliyesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Moto hautoacha kuendelea kuuliza juu ya zaidi mpaka pale Atapouweka unyayo Wake. Hapo ndipo ukusanyike na useme: “Tosha, tosha.”

  • Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-us-Swifaat, uk. 40-41
  • Imechapishwa: 21/10/2017