3- Yanayoruhusu kwa mfanyaji I´tikaaf
Inaruhusu kwa aliyekaa I´tikaaf kutoka nje ya msikiti kwa yale mambo ambayo hakuna budi ayafanye. Mfano wa kutoka kwa ajili ya kula na kunywa akiwa hana mtu wa kumletea, kukidhi haja, kutawadha kutokamana na hadathi na kuoga janaba.
Anaruhusiwa kuzungumza na watu kwa mambo yenye faida na kuulizia hali zao. Ama kuzungumza mambo yasiyokuwa na faida na mambo yasiyokuwa na dharurah ni mambo yanayopingana na malengo ya I´tikaaf na yaliyosuniwa kwa ajili yake. Inaruhusu kwa baadhi ya wakeze na nduguze kumtembelea, wakamzungumzisha kwa kitambo fulani na akatoka katika I´tikaaf yake kwa ajili ya kuwaaga. Swafiyyah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa amekaa I´tikaaf ambapo nikamjia wakati wa usiku, nikamzungumzisha, halafu nikainuka na kugeuka. Akasimama kwa ajili ya kunisindikiza… “[1]
Bi maana anamsindikiza nyumbani kwangu.
[1] al-Bukhaariy (2035) na Muslim (2175).
- Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 169-170
- Imechapishwa: 04/05/2021
3- Yanayoruhusu kwa mfanyaji I´tikaaf
Inaruhusu kwa aliyekaa I´tikaaf kutoka nje ya msikiti kwa yale mambo ambayo hakuna budi ayafanye. Mfano wa kutoka kwa ajili ya kula na kunywa akiwa hana mtu wa kumletea, kukidhi haja, kutawadha kutokamana na hadathi na kuoga janaba.
Anaruhusiwa kuzungumza na watu kwa mambo yenye faida na kuulizia hali zao. Ama kuzungumza mambo yasiyokuwa na faida na mambo yasiyokuwa na dharurah ni mambo yanayopingana na malengo ya I´tikaaf na yaliyosuniwa kwa ajili yake. Inaruhusu kwa baadhi ya wakeze na nduguze kumtembelea, wakamzungumzisha kwa kitambo fulani na akatoka katika I´tikaaf yake kwa ajili ya kuwaaga. Swafiyyah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa amekaa I´tikaaf ambapo nikamjia wakati wa usiku, nikamzungumzisha, halafu nikainuka na kugeuka. Akasimama kwa ajili ya kunisindikiza… “[1]
Bi maana anamsindikiza nyumbani kwangu.
[1] al-Bukhaariy (2035) na Muslim (2175).
Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 169-170
Imechapishwa: 04/05/2021
https://firqatunnajia.com/04-yanayoruhusu-kwa-anayefanya-itikaaf/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)