04. Ni ipi hukumu ya kula daku baada ya kuingia alfajiri?

Swali 04: Ni ipi hukumu ya mwenye kula daku baada ya wakati?

Jibu: Inategemea na daku ilikuliwa lini. Ikiwa limetokea baada ya wakati kwa muda mrefu basi inatakiwa kulipwa tena. Na ikiwa limetokea isiyozidi dakika tano ni lenye kusamehewa – Allaah akitaka.

Kunapoingia alfajiri ya pili ndio imeharamishwa kula na kujuzu kuswali Fajr. Ratiba ya muda haiko mia kwa mia sawa. Inaonekana kuwa ratiba ya muda imefanywa kwa ajili tu ya usalama zaidi. Iwapo mtu ataswali baada tu ya adhaana ya Fajr tunasema kuwa swalah yake si sahihi. Ni wajibu kwake kuswali tena kwa sababu ameswali kabla ya wakati kuingia.

Kwa kifupi ni kwamba anatakiwa kuiangalia hali yake. Ikiwa alikula daku baada ya muda mrefu uliyoko kwenye ratiba ya muda ni wajibu kuilipa siku hiyo.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaas-Swiyaam, uk. 20-21
  • Imechapishwa: 11/06/2017