1. Anayotakiwa kufanya mambo ambayo ni maumbile ya Kiislamu katika mambo ambayo ni maalum kwake na yanafanana na yeye:
a) Kupunguza kucha na kuzipatiliza kwa kuzikata mara kwa mara. Kwa sababu kukata kucha ni Sunnah kwa maafikiano ya wanachuoni. Ni miongoni mwa mambo ya maumbile ya Kiislamu yaliyopokelewa katika Hadiyth. Jengine kuyaondosha ndio usafi na uzuri. Kuyabakiza yakawa marefu kunamfanya mtu akaonekana vibaya na pia kujifananisha na wanyama, kukusanya uchafu chini yake na kuzuia maji kufika chini yake.
Baadhi ya wanawake wa Kiislamu wamepewa mtihani wa kufuga kucha zao kwa ajili ya kujifananisha na wanawake wa kikafiri na kuwa wajinga juu ya Sunnah.
b) Imesuniwa kwa mwanamke kuondosha nywele za kwapani na za sehemu ya siri kwa ajili ya kutendea kazi Hadiyth iliopokelewa katika jambo hilo na kutokana na ule uzuri unaopatikana katika jambo hilo. Lililo bora ni yeye afanye hivo kila wiki au asiziache zaidi ya siku arubaini.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 17
- Imechapishwa: 21/10/2019
1. Anayotakiwa kufanya mambo ambayo ni maumbile ya Kiislamu katika mambo ambayo ni maalum kwake na yanafanana na yeye:
a) Kupunguza kucha na kuzipatiliza kwa kuzikata mara kwa mara. Kwa sababu kukata kucha ni Sunnah kwa maafikiano ya wanachuoni. Ni miongoni mwa mambo ya maumbile ya Kiislamu yaliyopokelewa katika Hadiyth. Jengine kuyaondosha ndio usafi na uzuri. Kuyabakiza yakawa marefu kunamfanya mtu akaonekana vibaya na pia kujifananisha na wanyama, kukusanya uchafu chini yake na kuzuia maji kufika chini yake.
Baadhi ya wanawake wa Kiislamu wamepewa mtihani wa kufuga kucha zao kwa ajili ya kujifananisha na wanawake wa kikafiri na kuwa wajinga juu ya Sunnah.
b) Imesuniwa kwa mwanamke kuondosha nywele za kwapani na za sehemu ya siri kwa ajili ya kutendea kazi Hadiyth iliopokelewa katika jambo hilo na kutokana na ule uzuri unaopatikana katika jambo hilo. Lililo bora ni yeye afanye hivo kila wiki au asiziache zaidi ya siku arubaini.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 17
Imechapishwa: 21/10/2019
https://firqatunnajia.com/04-kukata-kucha-na-kuondosha-nywele-za-kwapani-na-sehemu-ya-siri/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)