04- ´Aliy bin ´Abdillaah bin Muyassir ametuhadthia: Abul-Ash´ath Ahmad bin al-Miqdaam ametuhadthia: Muhammad bin ´Abdir-Rahmaan at-Twafaawiy: Ayyuub ametuhadthia, kutoka kwa Muhammad, kutoka kwa Abu Hurayrah, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Pepo na Moto vilizozana ambapo Moto ukasema: “Ndani yangu wanaingia wakandamizaji na wenye kiburi.” Pepo nayo ikasema: “Ndani yangu wanaingia watu wadhaifu na wale masikini.” Ndipo Allaah (´Azza wa Jall) akasema: “Wewe ni adhabu Yangu ambayo namsibu yule Ninayemtaka.” Akasema kuiambia Pepo: “Wewe ni huruma Yangu ambayo namsibu yule Ninayemtaka. Kila mmoja wenu atajazwa.” Itapofika siku ya Qiyaamah basi Allaah (´Azza wa Jall) hatomdhulumu yeyote katika waja Wake kitu chochote. Kutatupwa Motoni na useme:
هَلْ مِن مَّزِيدٍ
“Hakuna zaidi?”[1]
Mpaka Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) aweke unyayo Wake. Hapo ndipo utajaa, ukusanyike na useme: “Tosha, tosha.”
[1] 50:30
- Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-us-Swifaat, uk. 39-40
- Imechapishwa: 18/10/2017
04- ´Aliy bin ´Abdillaah bin Muyassir ametuhadthia: Abul-Ash´ath Ahmad bin al-Miqdaam ametuhadthia: Muhammad bin ´Abdir-Rahmaan at-Twafaawiy: Ayyuub ametuhadthia, kutoka kwa Muhammad, kutoka kwa Abu Hurayrah, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Pepo na Moto vilizozana ambapo Moto ukasema: “Ndani yangu wanaingia wakandamizaji na wenye kiburi.” Pepo nayo ikasema: “Ndani yangu wanaingia watu wadhaifu na wale masikini.” Ndipo Allaah (´Azza wa Jall) akasema: “Wewe ni adhabu Yangu ambayo namsibu yule Ninayemtaka.” Akasema kuiambia Pepo: “Wewe ni huruma Yangu ambayo namsibu yule Ninayemtaka. Kila mmoja wenu atajazwa.” Itapofika siku ya Qiyaamah basi Allaah (´Azza wa Jall) hatomdhulumu yeyote katika waja Wake kitu chochote. Kutatupwa Motoni na useme:
هَلْ مِن مَّزِيدٍ
“Hakuna zaidi?”[1]
Mpaka Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) aweke unyayo Wake. Hapo ndipo utajaa, ukusanyike na useme: “Tosha, tosha.”
[1] 50:30
Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kitaab-us-Swifaat, uk. 39-40
Imechapishwa: 18/10/2017
https://firqatunnajia.com/04-dalili-juu-ya-mguu-wa-allaah-4/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)