03. Faradhi ya kwanza kwa watoto

وأول ما فرض الله على عباده الكفر بالطاغوت والإيمان بالله، قال تعالى

Kitu cha kwanza Allaah kukifaradhisha kwa waja ni kukufuru Twaaghuut na kumuamini Allaah. Allaah (Ta´ala) amesema:

وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ

“Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Mtume [awaamrishe watu wake] kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaaghuut.”[1]

والطاغوت: ما عبد من دون الله أو الشيطان، والطاغوت، والكهانة، والمنجم، ومن يحكم بغير ما أنزل الله، وكل متبوع مطاع على غير الحق

Twaaghuut ni:

1- Kila chenye kuabudiwa badala ya Allaah.

2- Shaytwaan.

3- Kuhani.

4- Mnajimu.

5- Anayehukumu kinyume na aliyoteremsha Allaah.

6- Kila mwenye kufuatwa na kutiiwa katika kitu kisichokuwa haki.

قال العلامة ابن القيم رحمه الله تعالى: الطاغوت: ما يجاوز به العبد حده من معبود، أو متبوع، أو مطاع

´Allaamah Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:

Twaaghuut ni kila chenye kuabudiwa, kufuatwa na kutiiwa ambacho mja amepindukia kwacho mipaka.”[2]

[1] 16:36

[2] I´laam-ul-Muwaqqi´iyn (1/5).

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ta´liym-us-Swibyaan at-Tawhiyd, uk. 15-16