1054- Vilevile yeye huyohuyo amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa katika safari ambapo akamuona bwana mmoja watu wamekusanyika juu yake na wamemfanyia kivuli ambapo akasema: “Ana nini huyu?” Wakasema: “Ni mtu amefunga.” Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Si wema kufunga safarini.”[1]
Katika upokezi mwingine kumezidishwa:
“Lazimianeni na ruhusa ya Allaah ambayo amekupeni.”[2]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Si katika wema kufunga safarini.”
Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud na an-Nasaa’iy.
Katika upokezi wa an-Nasaa´iy imekuja:
“Hakika Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimpitia bwana mmoja aliyekuwa chini ya kivuli cha mti na akinyunyiziwa maji. Akasema: “Ana nini rafiki yenu?” Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Amefunga.” Ndipo akasema: “Hakika si katika wema mkafunga katika safari. Lazimianeni na ruhusa ya Allaah aliyokupeni na muikubali.”[3]
[1] Swahiyh.
[2] Ziada hiyo ipo kwa an-Nasaa´iy peke yake. Nimeyataja hayo katika “Irwaa’-ul-Ghaliyl” (4/54-57).
[3] Swahiyh.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/614-615)
- Imechapishwa: 21/04/2020
1054- Vilevile yeye huyohuyo amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa katika safari ambapo akamuona bwana mmoja watu wamekusanyika juu yake na wamemfanyia kivuli ambapo akasema: “Ana nini huyu?” Wakasema: “Ni mtu amefunga.” Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Si wema kufunga safarini.”[1]
Katika upokezi mwingine kumezidishwa:
“Lazimianeni na ruhusa ya Allaah ambayo amekupeni.”[2]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Si katika wema kufunga safarini.”
Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud na an-Nasaa’iy.
Katika upokezi wa an-Nasaa´iy imekuja:
“Hakika Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimpitia bwana mmoja aliyekuwa chini ya kivuli cha mti na akinyunyiziwa maji. Akasema: “Ana nini rafiki yenu?” Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Amefunga.” Ndipo akasema: “Hakika si katika wema mkafunga katika safari. Lazimianeni na ruhusa ya Allaah aliyokupeni na muikubali.”[3]
[1] Swahiyh.
[2] Ziada hiyo ipo kwa an-Nasaa´iy peke yake. Nimeyataja hayo katika “Irwaa’-ul-Ghaliyl” (4/54-57).
[3] Swahiyh.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/614-615)
Imechapishwa: 21/04/2020
https://firqatunnajia.com/02-hadiyth-hakika-si-katika-wema-mkafunga-katika-safari/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)